Unit 35

Somo La Thelathini Na Tano
Kutafuta Msaidizi: Looking for an Assistant

Original Audio (based on 1988 edition of textbook)

Mazungumzo

1. Listen to the whole dialog

2. Repeat after one speaker

3. Repeat after two speakers

Mazoezi

1. Zoezi la kwanza

2. Zoezi la pili

3. Zoezi la tatu

4. Zoezi la nne

5. Zoezi la tano

6. Zoezi la sita

Supplementary Audio (for 2001 edition of textbook)

Mazungumzo

1a. Listen to the dialog

1b. Repeat after the speakers

Somo

Vocabulary

Vocabulary list part 1

Vocabulary list part 2

Mazungumzo (1988 version)

The text is included here to aid students using the 2001 edition of the text with the original audio based on the 1988 edition. Copyright Sharifa Zawawi.

Asha: Hasani, je utapenda kufanya kazi kwangu?
Hasani:Nitapenda lakini kwanza niambie kuna kazi za namna gani?
Asha: Kazi zote za nyumba. Uliwahi kufanya kazi popote?
Hasani: Naam. Nilikuwa nikifanya kazi kwa Bwana Cotes. Mwalimu mkubwa wa chuo cha ualimu.
Yeye ni mwalimu aliyetoka Canada.
Asha: Ulimfanyia kazi kwa muda gani?
Hasani: Nilikaa kwake miaka yote mitatu aliyokuwa hapa.
Asha: Basi unazifahamu kazi zote za nyumba. Kazi zangu kama kunipikia, kunisafishia nyumba,
kunifulia, kuniendea sokoni na kunifanyia kazi za bustani. Utaziweza kazi zote hizi?
Hasani: Ndiyo, nitaziweza. Nilikuwa nikimfanyia Bwana Cotes kazi hizohizo.
Asha: Vizuri sana. Mshahara wako utakuwa kiasi gani? Mimi ni peke yangu hapa kwa hiyo sitakuhitaji (sitakuhitajia - siyo sahihi) kutwa. Unaweza kunifanyia kazi kwa muda wa saa chache tu kila siku. Unataka nije saa ngapi na kwa muda gani kila siku?
Hasani: Itakuwa vizuri ikiwa utaweza kufika hapa asubuhi saa moja ili unitengenezee chakula cha asubuhi, na utaweza kuondoka saa sita za mchana.
Hasani: Hutaki nirudi jioni kukutengenezea chakula cha usiku?
Asha: Hapana nitakuwa nikila hoteli.
Hasani: Je, wewe utapendelea kunipa kiasi gani?
Asha: Unaonaje nikikupa shilingi mia na hamsini kwa mwezi. Zitakutosha?