Unit 38

Somo La Thelathini Na Nane
Mchezo Wa Soka: The Football Game

Original Audio (based on 1988 edition of textbook)

Mazungumzo

1. Listen to the whole dialog

2. Repeat after one speaker

3. Repeat after two speakers

Mazoezi

1. Zoezi la kwanza

2. Zoezi la pili

3. Zoezi la tatu

4. Zoezi la nne

5. Zoezi la tano

6. Zoezi la sita

Supplementary Audio (for 2001 edition of textbook)

Mazungumzo

1a. Listen to the dialog

1b. Repeat after the speakers

Vocabulary

Vocabulary list part 1

Vocabulary list part 2

Mazungumzo (1988 version)

The text is included here to aid students using the 2001 edition of the text with the original audio based on the 1988 edition. Copyright Sharifa Zawawi.

Juma: Jana nilikwenda mpirani. Si mpira huo ulikwenda?
Ana: La sikwenda. Je mpira ulikuwaje?
Juma: Ulikosa mambo. Kwani wewe si mtazamaji wa mpira?
Ana: Hutokea nikaenda mara nyingine.
Juma: Ningalijua kuwa ulitaka kwenda basi ningalikuambia tufuatane.
Ana: Hebu nieleze, mpira ulikuwaje?
Juma: Mpira ulikuwa u moto. Watu walishindana, waligombana, walisukumana hata walikaribia kupigana.
Ana: Lo! Basi kweli nilikosa mambo.
Wachezaji walikuwa ni nani?
Juma: Wachezaji wa Dar es salaam walipambana na wachezaji wa Unguja.
Ana: Walioshinda ni nani? Timu ya Unguja?
Juma: Hapana. Waliocheza vizuri sio walioshinda, na walioshinda hawakucheza vizuri. Timu ya Dar es salaam ilipata magoli matano kwa matatu ya wachezaji wa Unguja.
Ana: Ukienda Ijumaa ijayo tafadhali niarifu na mimi. Nitapenda kufuatana nawe.
Juma: Ningalijua unataka kwenda jana ningalikupitia.
Ana: Jana nisingaliweza kwenda kwa sababu nilikuwa na shughuli nyingine.