Somo La Ishirini Na Tisa
Safari kwa basi: "A Journey by Bus"
Original Audio (based on 1988 edition of textbook)
Mazungumzo
2. Repeat after one speaker
3. Repeat after two speakers
Mazoezi
2. Zoezi la pili
3. Zoezi la tatu
4. Zoezi la nne
5. Zoezi la tano
Supplementary Audio (for 2001 edition of textbook)
Mazungumzo
1b. Repeat after the speakers
Somo
Vocabulary
Vocabulary list part 2
Mazungumzo (1988 version)
Asha: Nataka kwenda Kisumu, naweza kwenda kwa basi?
Juma: Ndiyo unaweza lakini bora uende kwa treni.
Asha: La, sitaki kwenda kwa treni, nitapenda niende kwa basi ikiyumkinika.
Tikiti kiasi gani?
Juma: Tikiti ya kwenda na kurudi?
Asha: Tikiti ya kwenda tu.
Juma: Nauli ni shilingi ishirini na tano.
Asha: Ni umbali gani kutoka hapa mpaka huko?
Juma: Ni mwendo wa saa nne unusu. Utapenda kwenda wakati gani?
Asha: Basi la asubuhi huondoka (saa ngapi)? (lini - siyo sahihi)
Juma: Huondoka saa nne kamili na hufika saa nane na nusu
Asha: Basi litaondokea mahali gani?
Juma: Lazima ufike hapa saa tatu unusu ili upate kiti kizuri.
Asha: Nipande basi nambari gani?
Juma: Panda basi lolote kutoka kituo nambari tatu.
Asha: Ni ruhusa nichukue mizigo yoyote?
Juma: Una mizigo mingapi kwa jumla?
Asha: Nina mizigo miwili,s mmoja mkubwa na mmoja mdogo. Ninaweza kuichukua yote miwili?
Juma: Oo ndiyo, bila shaka unaweza kuichukua.
Asha: Niteremke mahali gani?
Juma: Teremka stesheni ya kisumu.