Unit 27

Somo La Ishirini Na Saba
Utasafiri Afrika ya Mashariki lini? When will you travel to East Africa?

Original Audio (based on 1988 edition of textbook)

Mazungumzo

1. Listen to the whole dialog

2. Repeat after one speaker

3. Repeat after two speakers

Mazoezi

1. Zoezi la kwanza

2. Zoezi la pili

3. Zoezi la tatu

4. Zoezi la nne

5. Zoezi la tano

6. Zoezi la sita

Supplementary Audio (for 2001 edition of textbook)

Mazungumzo

1a. Listen to the dialog

1b. Repeat after the speakers

Somo

Vocabulary

Vocabulary list part 1

Vocabulary list part 2

Mazungumzo (1988 version)

The text is included here to aid students using the 2001 edition of the text with the original audio based on the 1988 edition. Copyright Sharifa Zawawi.

Asha: Utasafiri Afrika ya Mashariki lini?
Juma: Nitasafiri Agosti tisa mwaka huu. Ningalisafiri Januari, lakini hali ya hewa so mzuri wakati huo.
Asha: Utakwenda mji gani?
Juma: Nitakwenda Nyeri na ningalipenda kufika Lamu na Mombasa.
Asha: Nyeri iko sehemu gani Afrika ya Mashariki?
Juma: Nyeri ni mji mmoja wa Kenya na uko karibu na Nairobi.
Asha: Utakwenda na nani, peke yako?
Juma: Nitakwenda pamoja na bibi yangu na watoto wetu watatu.
Asha: Mtasafiri vipi, kwa ndege?
Juma: Tutasafiri kwa ndege mpaka Nairobi, halafu kwa motokaa mpaka Nyeri.
Asha: Mnatumai kufanya nini huko?
Juma: Mimi nitafundisha katika Chuo cha Ualimu na bibi yangu atafanya kazi za nyumbani na labda atasaidia katika chama cha umoja wa wanawake.
Asha: Je watoto, wataweza kuingia shule?
Juma: Nafikiri wataweza kupata. Labda watajifunza katika shule ya Kenyatta.
Asha: Ndege itapita miji gani na safari yenu itachukua muda gani?
Juma: Nafikiri itapita Dakar, Lagos na Entebbe. Safari nzima itachukua kiasi cha saa kumi na nane. Je utapenda kuja pamoja nasi?
Asha: Ningependa kuja lakini sina nafasi mwaka huu. Kwani nyinyi mtakaa huko kwa muda gani?
Juma: Labda miaka miwili, hatujui bado.
Asha: Mtarudi America?
Juma: Tutarudi tukijaaliwa baada ya miaka miwili au zaidi ya miaka miwili.