Unit 39

Somo La Thelathini Na Tisa
Mbugani: At the National Park

Original Audio (based on 1988 edition of textbook)

Mazungumzo

1. Listen to the whole dialog

2. Repeat after one speaker

3. Repeat after two speakers

Mazoezi

1. Zoezi la kwanza

2. Zoezi la pili

3. Zoezi la tatu

4. Zoezi la nne

5. Zoezi la tano

6. Zoezi la sita

7. Zoezi la saba

8. Zoezi la nane

9. Zoezi la tisa

Supplementary Audio (for 2001 edition of textbook)

Mazungumzo

1a. Listen to the dialog

1b. Repeat after the speakers

Vocabulary

Vocabulary list part 1

Vocabulary list part 2

Vocabulary list part 3

Mazungumzo (1988 version)

The text is included here to aid students using the 2001 edition of the text with the original audio based on the 1988 edition. Copyright Sharifa Zawawi.

Scott: Jambo gani lililokufurahisha katika safari yako.
Asha: Kwa muda mrefu nilitamani kuizuru mbuga ya Serengeti ili niweze kuwaona wale
wanyama waonekanao kwenye sinema zetu siku zote. Nilipopata likizo yangu
(likizo yangu is the right word - not likizo langu) nilifunga safari kwenda Tanzania.
Scott: Uliona nini huko tafadhali nieleze.
Asha: Mandhari ya mbuga hiyo ni ya kustaajabisha. Uwanda unaotandazika kiasi cha maili
elfu sita za eneo. Kimo cha ardhi ni futi elfu tatu mpaka elfu sita hivi. Tulifurahi sana kuona wanyama
wa aina mbalimbali wametawanyika kila mahali.
Scott: Ulikwenda lini?
Asha: Tulikwenda katika mwezi wa juni kwa hivyo hali ya hewa ilikuwa nzuri. Tuliona wanyama wa
kila aina ambao sijapata kuwaona maisha yangu yote:- simba, tembo, viboko, twiga, vifaru, nyati, nyumbu, paa, chui na wengineo.
Scott: Wanyama hawa wana faida yoyote kwa nchi?
Asha: Wanyama hawa wa asili huiletea nchi mandhari ya kupendeza, mafundisho ya maana
kwa watazamaji na ni uchumi wa faida kwa serikali.