Unit 37

Somo La Thelathini Na Saba
Mgeni anakaribishwa: A guest is welcomed.

Original Audio (based on 1988 edition of textbook)

Mazungumzo

1. Listen to the whole dialog

2. Repeat after one speaker

Mazoezi

1. Zoezi la kwanza

2. Zoezi la pili

3. Zoezi la tatu

4. Zoezi la nne

5. Zoezi la tano

Supplementary Audio (for 2001 edition of textbook)

Mazungumzo

1a. Listen to the dialog

1b. Repeat after the speakers

Somo

Vocabulary

Vocabulary list part 1

Vocabulary list part 2

Vocabulary list part 3

Mazungumzo (1988 version)

The text is included here to aid students using the 2001 edition of the text with the original audio based on the 1988 edition. Copyright Sharifa Zawawi.

Bakari: Karibu, karibu bwana Anders.
Anders: Starehe, bwana Bakari. Je habari za siku nyingi?
Bakari: Salama tu. Je na wewe uhali gani? Hatukukuona kitambo sasa.
Anders: Mzima ila kazi zilinishughulisha kidogo. Nyumba yako nzuri
na mapambo yake yamependeza sana.
Bakari: Ahsante. Ni kazi ya bibi yangu. Yeye atakuja sasa hivi. Anamlaza
mtoto wetu mdogo. Huyu ni rafiki wangu bwanaMhina.
Naye pia anafundisha na anafanya kazi nawe bwana katika Wizara ya Elimu.
Anders: Nimefurahi kuonana nawe bwana.
Mhina: Na mimi pia nimefurahi kuonana nawe.
Je, upo kitambo hapa mjini?
Anders: Ni wiki hivi mbili tangu nifike.
Mhina: Umekwisha uona mji wetu? Unauonaje? Umekupendeza?
Anders: Naam. Nimeupenda sana lakini bado sijauona vyema.
Bakari: Bwana Anders, tafadhali njoo nikujulishe na bibi wangu. Huyu ni mama wa watoto, Fatuma.
Anders: Hujambo bibiye?
Fatuma: Sijambo bwana. Habari za Sweden?
Anders: Nzuri lakini ni kitambo tangu niondoke huko.
Fatuma: Niwie radhi sikuwapo hapa kukaribisha ulipofika. Nilikuwa nikimlaza mtoto.
Anders: Si kitu. Watoto hawajambo?
Fatuma: Hawajambo wamekwisha kuamkia? Mtoto wetu mdogo haoni vizuri.
Mwenziwe alimuangusha ngazini, akajiumiza kidogo mguu.
Anders: Maskini, hajambo sasa?
Fatuma: Hajambo.
Bakari: Hawa ni watoto wetu wengine Shabani na Rajabu.
Rajabu: Shikamoo bwana.
Shabani:Shikamoo bwana.
Anders: Marahaba, hamjambo?
Shabani na Rajabu: Hatujambo.
Anders: Mna watoto wazuri sana.
Bakari: Kweli wazuri lakini watundu mno. Kutwa wanamtaabisha mama yao.
Utapenda kunywa nini bwana Anders?
Anders: Kuna kinyaji gani?
Bakari: Kuna wiski, jin, bia, kokakola na maji ya machungwa.
Anders: Nitapenda maji ya machungwa tafadhali.
Bakari: Na barafu?
Anders: La, bila barafu.
Fatuma: Chakula ki tayari. Bwana wakaribishe wageni mezani.
Bakari: Tukisha kula tutakwenda mjini tukamtembeze mgeni tumuonyeshe mji wetu ulivyo.
Anders: Asante sana bwana lakini msijitaabishe sana.
Bakari: Utatufurahisha ukikubali kwenda.
Fatuma: Tafadhali ongezeni chakula.
Anders: Chakula kizuri na kitamu lakini nimeshiba sana. Umetuisha na kutunywisha bila kiasi.