Mwalimu: Una ndugu wangapi Juma?
Juma: Nina ndugu watatu.
Mwalimu: Wanaume wangapi na wanawake wangapi?
Juma: Wanawake wawili na mwanamume mmoja.
Mwalimu: Kaka yako ameoa?
Juma: Ndio ameoa, ana mke na watoto wawili.
Mwalimu: Je yeye anafanya kazi gani?
Juma: Yuko Chuo Kikuu cha Dar es salaam anajifunza kuwa Mwanasheria.
Mwalimu: Ndugu zako wa kike wameolewa?
Juma: Mmoja ameolewa na mmoja bado.
Mwalimu: Wao wanafanya nini?
Juma: Mmoja anasoma shule ya chini na mmoja anafanya kazi ya uuguzaji.
Mwalimu: Wazazi wako wanafanya nini?
Juma: Mama hafanyi kazi lakini baba ni mwalimu.